JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Mdau wa JamiiForums analalamika kuwa alitumia dawa za kutibu Ugonjwa wa Malaria zinazoitwa EKELFIN ambazo baadaye zilimsababishia kupatwa na mchubuko sehemu za siri na midomoni. Anashangaa kwanini Serikali haitoi taarifa kwa watumiaji juu ya madhara ya dawa hizi kwa binadamu. Ni kweli kuwa dawa hizi zinaweza kusababisha athari tajwa?
Katika jamii yetu ya kitanzania asilimia kubwa inatumia vyombo vya plastiki kunywea na kulia chakula, lakini nimekuwa nikisikia kuwa plastiki ina madhara makubwa kwa afya ya binadamu, wapo wanaodai inasababisha saratani, wengine inamaliza nguvu za kiume kwa wanaume na mambo mengi. Je, ni kweli ina madhara? Maana napata mashaka kwani sijawahi kusikia serikali ikisema kuhusu madhara hayo au kukemea matumizi yake wala kutoa elimu ya namna ya kuvitumia.
Alhamisi ya pili ya Mwezi Machi kila mwaka, Dunia huadhimisha Siku ya Figo Duniani ili kutoa ufahamu na kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa afya ya figo na magonjwa yanayohusiana na figo. Kupitia maadhimisho haya, watu hupata fursa ya kujifunza kuhusu njia za kuzuia magonjwa ya figo, kudhibiti magonjwa ya figo, na umuhimu wa kuwa na maisha yenye afya ya figo. Aidha, maadhimisho haya huchangia katika kuongeza uelewa wa umma kuhusu haja ya kuchangia katika juhudi za kuzuia na kutibu magonjwa ya figo, pamoja na kusaidia watu wenye matatizo ya figo kupata msaada unaohitajika. Hata hivyo, ugonjwa huu huambatana na dhana nyingi potofu zinazofifisha kasi ya kupambana nao hivyo JamiiCheck imekuandalia ufafanuzi wa Dhana hizo kama sehemu ya...
Imezoeleka kuona watoto wachanga wakiwa wamefunikwa manguo mengi sana, hii sio shida iwapo hali ya hewa inaruhusu yaani ya ubaridi au ya kawaida. IIa kunaweza kuwa na hali ya joto kali watu wazima mnatamani kukaa kwenye feni ila mtoto mchanga bado kafunikwa mablanketi na kavishwa sweta, ukihoji unajibiwa watoto wachanga hawahisi joto. Wapo wanaotetea hoja hii kwa madai tumboni kulikuwa na joto hivyo mtoto hawezi hisi joto bali huhisi baridi muda wote. Je, hii ni kweli?
Katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo katika jukwaa la JamiiForums.com, kumekuwa na majadiliano na maswali yanahoji au kutoa taarifa ambazo wengi hawana uthibitisho nazo kuhusu dawa za kuzuia maambukizi ya VVU ambazo muhusika anatakiwa kutumia ndani ya masaa 72. Je, hili lina ukweli? Na inakuaje kwa muhitaji ambaye si muhanga, na gharama zake zikoje? Je, kuna ukweli kwenye hili?
Kuna video inasambaa twiter na Instagram ikimuonesha mwanaume akiruka dirisha na kukimbia huku akiwa mtu kabisa bila nguo, watu hao wamekuwa wakishare video hiyo na kuweka ujumbe wa MKE WA MTU SUMU wakimaanisha mtu huyo alikuwa na mke wa mtu kisha akafumaniwa ndio anakimbia. Je, ni kweli mtu huyo anakimbia fumanizi na tukio hilo limetokea Tanzania? JamiiCheck, msaada wa kujua ukweli.
Salaam Wakuu, Ikiwa Ligi Kuu ya NBC imeisha leo 28/05/2024 huku Yanga akiwa Bingwa Azam nafasi ya pili na Simba nafasi ya tatu. Imetoka taarifa kuwa Simba Sports Club na Yanga SC zitacheza African Football League, Azam FC watacheza CAF Champions League pamoja na Coastal Union. Taarifa hiyo inadai Kombe la Shirikisho limefutwa. Je, kuna ukweli wowote wa taarifa hii?
Mara nyingi nikiwa na stress na kupelekea kukosa usingizi, huwa navuta sigara ili kupunguza stress hizo. Hata iwe usiku wa manane nitajitahidi niende kwenye Club zinazokesha nikafuate sigara. Suala la kuwa inanisaidia au lah, sidhani lakini pale napokuwa navuta huwa nakuwa katika hisia nyingine kabisa. Chanzo cha kutumia sigara kama relief ya stress, ni baada ya kuona kwenye muvi mara kwa mara, na ushauri kutoka kwa marafiki. Nachotaka kujua kitaalam ni kama kweli sigara inasaidia kupambana na msongo wa mawazo tunaokumbana nao mara kwa mara.
Kuna wazandiki huwa nawashangaa wanavyoponda pombe. Pombe haina madhara kama wanafiki wanavyotuaminisha. Pombe ni nzuri ukinywa kistaarabu, ina faida lukuki, ukibisha muulize Albert Chalamila. Tafiti zinasema kuwa beer zinasaidia kujilinda na magonjwa ya moyo. Kama mnavyojua magonjwa ya moyo yanaondoa watu kimya kimya hivyo mimi nawashauri tunywe beer kujilinda na magonjwa ya moyo. Hata Biblia inasisitiza tunywe pombe tufurahie, na mkituona tunakunywa pombe msitukwaze. Too much of anything is bad, but too much good whiskey is barely enough
Leo nimeona video ambao imewekewa sauti ya mtu akisema wametumiwa video hiyo kwenye group la shule ya Themihill, video hiyo inaonesha mtu akifungua kitu kinachoonekana kama pen (kalamu) ambacho ndani yake kina risasi na baadaye kufyatuliwa. Anayeelezea video hiyo anadai pen hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa huku akionesha hofu ya watoto kuuana au wao wenyewe kujidhuru kwa peni hizo. Ningependa kufahamu ukweli kuhusu video hiyo.
Back
Top Bottom